WANANCHI WANAPASWA KUIJUA NA KUISHIRIKI BAJETI YA NCHI

NAIBUMKURUGENZI wa Mtandao wa jinsia Tanzania TGNP Lilian Liundi amewataka watanzania kuijua bajeti ya nchi kisera na kisekta ili iwasaidie kutathimini na kuishiriki kwa kuhoji inapokuwa haitekelezeki.

Mbali na hilo pia ameishauri jamii kuzielewa vema sera za kisekta nchini ili kuwapa uwezo na urahisi wa kutambua mafanikio na changamoto zake ikiwa ni jia pekee ya kuharakisha upatikanaji wa maendeleo kupitia bajeti zilizopo.

Akifungua mafunzo wanawake ngazi ya jamii na waandishi wa habari katika ofisi za mtandao huo,Lilian alisema bajeti nyingi hazifikii malengo yake katika utekelezaji kutokana na uelewa mdogo juu ya bajeti hizo sambamba na umuhimu wake katika maisha ya kilasiku katika jamii.

“kumbukeni bajeti ni moja ya rasilimali muhimu katika maendeleo katika jamii na taifa kwsa jumla hivyo umuhimu wa kuifahamu na kuifuatilia kama inafanya kama ilivyokusudiwa ni lazima ili tuelewe tunanini kwa ajili ya nini na imefanya nini kwa kipindi kipi”alifafanua.

Akihimiza jamii kuunda vikundi maalumu kufuatilia bajeti hizo alivyo vita ‘vikundi vya mashujaa’ kufuatilia bajeti hizo, Lilian alisema jamii inapaswa kuwa mstari wa mbele kufuatilia kwa kina ikilinganisha kiasi ilichopokea na thamani yake kwenye utekelezaji miradi ya maendeleo.

“lakini pia jamii inapaswa kujua kuwa ulinganifu wa kijinsia ni muhimu sana hasa katika ufuatiliaji wa masuala haya muhimu ya kibajeti ili kupanuana mawazo katika kukabilia changamoto zinazojitokeza’aliongeza Lilian.

Awali mkuu wa taasisi ya mafunzo katika mtandao huo Ziki Mihyo aliwataka watanzania hususani wanawake kutengeneza mkakati wa ushawishi na utetezi katika masuala ya bajeti katika maeneo walipo ili utekelezwaji wake uende sambamba na matakwa ya sera na mahitaji ya jamii.

“kila mmoja anapaswa kutambua kuwa haki ya uchumi kwa jamii ni rasilimali zilizopo ziwanufaishe jamii “alisema Ziki.

Jumla ya wanawake,waandishi wa habari 35 kutoka vituo na vyombo mbalimbali vya habari nchini wapo jijini Dar es salaam katika mafunzo ya utambuzi wa bajeti na ushiriki wake katika kujiletea maendeleo ya kiuchumi kwenye jamii na taifa kwa jumla.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.