Jeshi lazingira makao ya polisi Lesotho
Ripoti kutoka Taifa la kusini
mwa Afrika Lesotho zinasema kuwa jeshi limezingira makao makuu ya polisi
na kuzuia matangazo ya radio pamoja na mtandao wa simu katika mji mkuu
wa Maseru.
Shirika la habari la AFP limemnukuu waziri wa
habari Thesele Maseribane akisema kuwa milio ya risasi ilisikika na
kukilinganisha kisa hicho na jaribio la mapinduzi.Uchaguzi ambao haukukamilika nchini humo miaka miwili iliopita ulisababisha kuundwa kwa serikali ya muungano isio dhabiti.
Licha ya mazungumzo ya kuleta amani mnamo mwezi Juni ,hali ya wasiwasi ilitanda huku majirani wa taifa hiilo wakionya dhidi ya mbinu yoyote isio ya kikatiba.
Taifa hilo limezungukwa na Afrika kusini na hutegemea sana jirani yake kwa mali asli pamoja na ajira.
Leave a Comment