Alshabaab wamteua kiongozi mpya



 
 Aliyekuwa kiongozi wa Al Shabaab Ahmed Godane


Kundi la wanamgambo la Al Shabaab limemtaja kiongozi wao mpya, baada ya aliyekuwa mwanzilishi wa kundi hilo Ahmed Godane kuuawa katika shambulizi lililofanywa na majeshi ya Marekani wiki ya jana.
Kiongozi huyo mpya wa sasa ni Ahmad Umar, ambaye kwa mujibu wa kamanda wa Al Shabaab Abu Mohammed, amesema uamuzi wa kumteua kiongozi huyo ulifikiwa bila pingamizi.
Katika taarifa ya kundi hilo, ilionya kutaka kulipiza kisasi mauaji ya kiongozi wao, na kusema hilo ni jukumu la Al Shabaab ambalo hawatawahi kukosa kutekeleza azma hiyo.
Aidha, mapema siku ya jumapili, waziri wa usalama wa ndani wa Marekani,amesema serikali yake imepokea taarifa za kundi hilo kupanga kushambulia vituo vya afya, elimu na taasisi zingine za serikali nchini humo.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.