Mahusiano ya kimapenzi ni kama moto wa kuni!!!!

Nakushukuru mdau wa blogger ya mahabati kwa kuendelea kufatilia makala mbalimbali za mahusiano ya kimapenzi, karibu tena katika makala nyingine ya mahusino ya kimapenzi ni kama moto wa kuni.
Unaweza ukajiuliza kwanini ninasema hivyo usipate jibu, au ukapata majibu tofauti na haya niliyo nayo katika makala hii ya mahusiano.
Kwa wale wenye kufahamu moto wa kuni ni mto mzuri sana kwa mapishi na wanawake wa vijijini wanajua raha ya moto huo, unaivisha mapema, hauna gharama kubwa kama mkaa, gesi, umeme, mafuta ya taa na nishati nyinginezo.
Kama ilivyo kawaida hakuna kilichokuwa na raha kikakosa karaha, ingawa karaha zinazidiana kulingana na kitu husika.
Moto wa kuni una moshi mwingi hasa ukikuta kuni mbichi, unasumbua kuwaka na kupuliza ni sehemu ya kuuchochea moto huu, wengine hadi macho hubadilika na kuwa mekundu kwa ajili ya moshi, taya nazo uuma kwa sababu ya kupuliza moto na vikamasi vepesi navyo huwa karibu haya yote ni ili chakula kiive mapema ndiyo maana nasema mahusiano ya mapenzi ni sawa na mto wa kuni.
Katika mahusiano ya mapenzi kuna bashasha nyingi ambazo zinahitajika ili kuendelea kuimarisha mahusiano yako ya kimapenzi na Yule umpendae na karaha nyingi ambazo huwafanya baadhi ya wanandoa kukata tamaa na kuwashawishi wengine kutodhubutu kuingia kwenye ndoa.
Bila kujua wapi alipokosea na nini anapaswa kufanya ili kuwa katika hali ya mahusiano imara yenye maisha ya umilele, kudhani suluhisho ni kuachana na mume au mke wake.
Kazi hii si ya mtu mmoja bali ya wote wawili ingawa watu wengine, hawana utamaduni wa kujua nini mwezake anahitaji na amtimizie kwa wakati gani na wapi alipokosea.
Ila ukweli usiyo pingika kuwa kama utapenda kutumia jiko la kuni lazima ukubali karaha zake na raha zake, na mahusiano yako ili yawe imara lazima uwe mwepesi wa kupenda kufanya yale mwezako anayokufanyia kwa maana kuwa inawezekana anapenda umfanyie ila anaona haya kukwambia.
Watu wametofautiana kimaumbile mpaka tabia hivyo, mapenzi siku zote hayataji ujuaji mwingi sana, ila yanataka ubunifu kama jiko la kuni, sasa kuna jiko la ukuni mmoja na kuna la kuni tatu, huu ni ubunifu wa jiko la kuni.
Jifunze kujinyima kwa ajili ya mume wako au mke wako ili kufanya angalau kitu kimoja ambacho kitakuwa cha kipekee sana katika mahusiano yenu na kitaendelea kuwa kumbukumbu isiyofutika.
Kuna jamaa mmoja wa huko uhaibuni alikuwa anatamani sana kumfanyia mambo mengi mke wake, lakini hakuwa na uwezo wa kufanya hivyo, alikusanya shilingi hamsini  kwa kila siku baada ya miaka kumi alikuwa anahela nzuri tu akaenda kumnunulia mke wake zawadi ambayo ilimfariji sana mkewe na kujiona kama vile ndiyo anachumbiwa.
Je wewe unafanya nini ili kuwa na mahusiano yenye kumbukumbu nyingi katika maisha yenu ya ndoa au umeridhika kwa kuwa umeshaoa au kuolewa?
Nawapongeza sana wanawake waliyo wengi ni hodari sana katika kuhakikisha wanawanunulia weza wao, zawadi mbalimbali, hata kama hana kazi atakuomba hela kwa madai ya kuwa na shida Fulani ili aweze kukununulia zawadi.
Lakini baadhi ya wanaume hujifunza na kuanza kufanya hivyo, na wengine hupuuza na kuona kama kuni mbichi ambazo hata uchochee bado zitatoa moshi.
Maisha ya mwanamke siku zote yamekuwa ya kipekee sana katika ndoa ingawa pia huingiliwa na mtihani wa ushindani wa kutaka kuwa wakipekee sana katika mahusiano.
Wanawake wengi wanakuwa wanachoka kwa kuona pengine zawadi anazotoa kwa mumewe hazifirahii na ndiyo maana anahindwa kujibu kwa kumpa na yeye zawadi.
Kwa hakika zawadi ni moja ya kichochezi kikubwa cha kuweza kumweka mtu aliye mbali karibu kimwili na hata kiakili na hii huwa kama deni ndani ya dhamira ya anayetoa kumbuka ukijua kupokea jua na kutoa.
Hiyo ni misemo ya zamani ila ina maana kubwa sana endapo utataka kujua maana yake je wewe umepokea mara ngapi vingapi umerudisha?

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.