MASWALI YA KUULIZANA WANANDOA WATARAJIWA KABLA YA KUOANA
1. Kwa nini unaoa/kuolewa?
2. Una uhakika uko tayari kwa ndoa?(sio harusi)?
3 Matarajio yako ni nini katika ndoa?
4 Mahitaji yako ni nini katika ndoa?
5. Ni sababu zipi zinaweza kukufanya uachane na mwenzio?
6. Vitu gani usivyopenda kutoka kwake?
7. Vitu gani unapenda kutoka kwake?
- Unapenda tuwe na watoto wangapi (Mungu akitujalia)
- Mungu asipotujalia mototo katika ndoa yetu utachukua hatua gani?
- Una maoni gani juu ya njia mbalimbali za uzazi wa mpango?
- Kama mimi nikipata kazi mbali na wewe unapofanya kazi tutaishije?
- Dini/dhehebu ikiwa tofauti na wewe tutafanyeje?
- Una malengo gani katika maisha yako?
- Unafikiri nini kuhusu talaka?
Hayani maswli machache tu,
lakini kupitia haya yataibuka maswali mengine mengi. Mwenzako anapokuuliza haya
maswali usifikiri hana upendo kwako au yuko"too judgementa". Lengo
lake ni kujua ataishi na mtu wa namna gani na hivyo ajiandae vipi. Maswali haya
yanaweza kuibua mawazo na hisia tofauti kati ya wapendanao, na yanapoibuka mawazo
na hisia za wawili hawa ndipo wanapozidi kujuana na kuziona tofauti zao za
kimtazamo juu ya mambo fulaani. Hii itawasaidia wao kujipanga kukabiliana na
tofauti zilizo ibuka wakati wa majadiliano.
Nawashauri vijana wenzangu wasioe au kuolewa kwa sababu tu wanataka kuoa au kuolewa. Ni muhimu wakawa na maandalizi katika akili yao (pre-marital mental preparation).
Nawashauri vijana wenzangu wasioe au kuolewa kwa sababu tu wanataka kuoa au kuolewa. Ni muhimu wakawa na maandalizi katika akili yao (pre-marital mental preparation).
Leave a Comment