NI MAKOSA KUAMINI KUWA NJIA ZA KUMFURAHISHA MWANAMKE AU MWANAUME KATIKA MAHUSIANO NA HASA TENDO LA NDOA ZINAFANANA.

Ni ukweli usiyopingika kuwa maisha ya leo ni tofauti na ya jana na siku ya leo ni tofauti na kesho, hii inadhirihika katika mahusiano ya leo.
Watu wengi wanaoingia katika mahusiano wanashindwa kuajua kuwa kila jambo lina wakati wake, kuna wakati wa kufurahi na wakati wa huzuni ila kila wakati una faida yake katika maisha.
Unapokuwa kwenye mahusiano lazima uwe na wakati wa kujua vema mweza wako ili ujue nini utafanya ili kumfurahisha pale anapokuwa katika huzuni.
Hali hii inakufanya uzidi kuwa mwanafunzi na upende somo la mahusiano ya kimapenzi kwa kuwa somo hili halina mkubwa wala mdogo, wote wanahitaji kujifunza kwa undani kadri siku zinavyokwenda.
Utakubaliana na mimi kuwa wanandoa wengi wanadhani kuwa tendo la ndoa au faragha inafumo maalumu, na ndiyo maana wengine hutwanga na kupepeta na wengine huona kama ukimshikashika mwanamke inatosha kumbe bado elimu ya ziada ina hitajika ili kufaulu somo hili lisilokuwa na ukomo katika kulisoma.
Mimi binafsi naamini kuwa maisha yanahitaji umakini mkubwa ili kufanikiwa, pamoja  na jitihada na kumwomba Mungu atuwezeshe kufika kule tunakotaka kwenda.
Ndivyo ilivyo katika mahusiano ni kosa la jinai kuona unajua kila kitu na kumbe hujui, jifanye ujui ili ujue, na onyesha kiu ya kutaka kujua ili ujulishwe, kusoma vitabu mbalimbali na kutembelea mitandao mbalimbali ya jamii.
Jitahidi hata kama umedumu katika mahusiano kwa miaka mingi tumia muda wako, kubuni mbinu mpya za mahusiano ili kumfurahisha mume wako au mke wako kudumisha amani katika mahusiano ni jambo la msingi.
Kuingia kwenye ndoa au mahusiano si kazi kazi ni kudumu katika mahusiano hayo, ila yote yanawezekana Endapo utamshirikisha Mungu nyakati zote bila kuchoka.
Na hii haijalisho ni mwanamke au mwanaume mnapaswa kushirikiana ili kubosresha ndoa yenu, kwa kuwa wabunifu na kujituma hata kama umechoka ndiyo siri ya mafanikio na kuendelea kufatilia www.brunokimaro.blogspot.com kwa Mahusiano Imara na salama.
Epuka kufanya mapenzi kwa kukariri kuwa huyu anapenda romance kumbe mwezio hapendi,  au unamtania mwenza wako kumbe  hapendi ila unafanya kwa mazoea epuka hilo.
Kwa kukubali kuwa wewe ni mwanafunzi siku zote uko darasani utajifunza mambo mapya.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.