Hii ya noti ya shilingi elfu moja Tanzania umeipata?.
Kumbukumbu
zako ziko sawa kuhusu yale malalamiko ya kukosewa kwa picha ya baba wa
taifa hayati Mwalimu Nyerere kwenye noti ya shilingi elfu moja? basi
kama hazipo sawa, ichukue hiyo.
Baada ya
hayo malalamiko unaambiwa Benki Kuu ya Tanzania imesema imeanza kufanyia
kazi malalamiko ya kukosewa kwa picha ya Rais wa kwanza wa Tanzania,
Marehemu Mwalimu Julius Nyerere ambapo mkurugenzi wa huduma za kibenki
Emmanuel Boaz amesema tayari benki hiyo imeanza kufanyia kazi hayo
malalamiko baada ya kusoma katika mitandao ya jamii.
Mwananchi
wameandika mkurugenzi huyo alisema BoT haijapata taarifa rasmi kutoka
kwa mtu yoyote lakini wameamua kuzifanyia kazi taarifa hizo “Na sisi
tumesoma katika mitandao, hakuna taarifa rasmi tuliyoipata lakini
hatuwezi kudharau tuhuma hizo na endapo tukigundua kuna matatizo
tutachukua hatua za kubadilisha haraka”
Kwa
mujibu wa mkurugenzi huyo, suala la picha kukosewa sio geni kwani
ilishawahi kutokea mara kadhaa kwa marais wastaafu na BoT ililazimika
kubadili haraka ili kutoharibu mtazamo wa Taifa ambapo alitoa mfano wa
picha ya Mwalimu Nyerere kukosewa na kuonekana nguo aliyovaa imefanana
na blauzi lakini pia picha ya Rais Ally Hassani Mwinyi ambayo ilionekana
shingoni ana mikunjo.
Kutokana
na hali hiyo, mkurugenzi huyo aliwatoa hofu Watanzania kuwa endapo
itabainika kama noti hizo zina kasoro zitarekebishwa ambapo hivi
karibuni, mitandao ya kijamii iliwakariri wanafamilia ya Rais huyo wa
kwanza wakilalamikia picha hiyo kwenye noti ya Sh1,000 kukosewa.
Leave a Comment