JIULIZE HAYA KWA FAIDA YA MAPENZI YAKO
Kupendana kwa dhati ni nguzo imara inayofanya mapenzi baina ya wapendanao yaweze
kuwa imara na madhubuti. Wanaopendana kwa dhati wanasikilizana, kuhesimiana na
kila mmoja kuwa na hamu na shauku na mwenzake.
Katika mapenzi hivyo ni vitu muhimu sana.
Ili mapenzi yaweze kustawi heshima inabidi iwepo baina ya wahusika. Ili kila
mmoja aweze kuwa na furaha na faraja katika mahusiano inabidi miongoni mwao
kuwepo na hamu na shauku. Mmoja akikosa hali hii mapenzi hukosa ladha. Si ajabu
kuona mwingine akianza kuhisi anajipendekeza kwa mwnenzake au kuona akikosa
raha kabisa ndani ya mahusiano hayo.
Wewe uko vipi kwa mpenzi wako?
Je, unampa
sababu ya kwenda kifua mbele kwa marafiki zake na kusema anamtu anayempenda kwa dhati? Umempa jeuri hiyo
mwenzako?Au ndiyo vile kila siku unamfanya asitamani kuwepo mapenzi katika
dunia!
Unafanya ajivunie kuwa katika mahusiano kama
wenzake anavyowasikia wakisema. Au umempa manung’uniko na ganzi ya moyo?
Ikiwa hukulazimishwa kuingia katika
mahusiano na uliyenaye hupaswi kumfanyia hivyo. Mapenzi ni faraja na burudani,
sasa kwanini unamfanyia hivyo mwenzako?
Hivi ulishawahi kujiuliza hatima ya lawama za
kila siku za mpenzi wako dhidi ya matendo yako yasiyoonesha dalili za mapenzi
wala kumjali? Tengeneza picha ya kitakachotokea baada ya mpenzi wako kuchoshwa
na hali hiyo. Hakuna binadamu anayependa kuteseka ikiwa kuna sehemu anahisi
atapata faraja na amani ya nafsi.
Je,
vipi kauli zako kwa mpenzi wako ni zile za kujenga tabasamu katika sura yake au
ni maudhi na fujo kwa kwenda mbele? Unamfanya mwenzako afurahi karibu kila neno
linalotoka katika kinywa chako, au ndiyo ukianza kuongea tu unamfanya alie na
kujutia hatua yako ya kufungua mdomo?
Maneno yako yanachangia asilimia ngapi ya
furaha katika maisha yake? Au ndiyo asilimia kubwa ya huzuni zake zipo katika
maneno yako.
Unampa sababu ya kukuamini? Au ndiyo ukitoka
tu yeye tumbo joto akifikiria kile alichokikuta katika simu yako! Yuko hivyo?
Chunga sana.
Ulishawahi kujiuliza mwisho wa wasi wasi wake
kwako nini? Unadhani kuna mtu anapenda kila siku kuwa roho juu? Fikiri upya kuhusu hili.
Wengi waliosalitiwa
na wapenzi
pia
sababu hii imo. Walivyoona wapenzi wao hawawaelewi waliamua kujipa pumziko la moyo kwa wengine,
kwa kile walichoaimini kama kupunguza aina ya
f’lani ya wasiwasi kwa maana kama ni ubaya basi wote watakuwa
wakifanyiana.
Kuwa makini zaidi katika mahusiano yako
ikiwa kweli unahitaji amani na burudani halisi. Ni mara ngapi mpenzi wako amewahi
kukutilia mashaka na f’lani hapo mtaani au kazini? Unadhani ni kwanini ana
mashaka hayo? Bila shaka ni ukaribu wenu uliojaa maswali. Ukaribu unaomnyima
raha na amani katika nafsi yake, kiasi cha kufanya ahisi anaibiwa mali yake.
Unaridhiwa
na wasiwasi wa mpenzi wako? Kwanini huchukui hatua za kumfanya ajue ukweli
halisi badala ya kumuacha aendelee kuteseka kwa mawazo na hangaiko la nafsi
kama si kweli?
Muite mpenzi wako pamoja na yule anaye
mshuku kisha mueleze ukweli halisi kama kweli mawazo yake si sahihi juu yenu.
Kumuacha
mpenzi wako apate msukosuko wa nafsi juu ya fikra zake juu ya ukaribu wenu ni
kumfanya kuamini kuwa ni kweli ‘mnatoka’ pamoja. Hata wewe bila shaka ungeamini
hivyo ingekuwa ni wewe.
Kuziacha hisia zake kuteseka ni kuonesha
kutomjali wala na kumthamini. Katika hali yoyote onesha thamani yake kwako kwa
matendo yako mazuri naya kutia faraja. Katika kila bonde weka sawa ili mapenzi
yenu yazidi kushamiri na kuongeza furaha baina yenu.
Leave a Comment