SABABU 10 KWANINI UMUACHE MWANAUME ULIYENAYE
2.
Upo
nae lakini kila mara unapowaza mipango yako ya baadae humuweki kwenye mipango
yako na hata unapokuwa unapokuwa naye mawazo yako muda mwingi yanakuwa mbali,
HUYO SI CHAGUO LAKO, Muache uendelee na safari.
3.
Kila
unapokuwa naye, Simu yake inakuwa yake na simu yako inakuwa yake pia, anasoma
sms na kuwa mkali sana kwenye simu yako ilhali yako wake huruhusiwi hata
kuigusa, HAKUFAI huyo ni Player, Trust Me.
4.
Kila
unapokuwa na ugomvi nae kila siku wewe ndio wa kumuomba msamaha hata kama yeye
ndio amekukosea, huyo hawezi kuwa na upendo wa kweli, mapenzi ni kusikilizana
pande zote mbili na si kwa upande mmoja kuonewa kwa kila kitu.
5.
Kuvaa
ni njia mojawapo ya kujiamini kwa mwanamke, lakini inapotokea anakupangia kila
vazi unalotakiwa kuvaa na usilotakiwa kuvaa hapo inakuwa sio sawa, huwezi
kutoka kwenda shule, kazini, outing, na kwingineko mpaka aone ulichovaa.
6.
Anakuchagulia
watu wa kuwa nao ikiwa ni pamoja na marafiki, hii sio dalili nzuri, wanaume
wanaotenda ‘’madhambi’’ pembeni ndo huwa na tabia hii kwa wingi, wewe unakuwa
ni mtu wa kubadili marafiki kila kukicha.
7.
Linapokuja
suala la pesa mara nyingi huwa hakuna undugu, mara nyingi amekuwa ni mtu wa
kukukopa pesa lakini anajifanya ‘’Kusahau’’ inapokuja muda wa kulipa deni, sio
dalili nzuri ya mwanaume anayekufaa, una mipango yako binafsi ukiachilia mbali
mapenzi na yeyote atakayesababisha mipango yako kutosogea mbele hatakiwi
kuvumiliwa.
8.
Mapenzi
yake kwako huongezeka pale tu anapokuhitaji kwa ajili ya kutimiza haja zake za
Ngono na anapomaliza hukusahau na kukupotezea, hakufai kabisa huyo mtu.
9.
Kila
unachomwambia hukusikiliza na kukubaliana nawe lakini inapokuja wakati wa
kutekeleza kwa vitendo mlichokubaliana mambo huwa tofauti, ANAKUDHARAU na
anajisemea moyoni ‘’Bora Liende’’, Hakufai.
10. Hawezi kila kitu cha
jikoni, hawezi kuosha vyombo hata kikombe cha chai, hawezi kupika hata chai,
hawezi hata kufua nguo zake za ndani na anaona kama kazi hizo zote ni za
wanawake tu, umejaribu sana kumuelekeza na haonyeshi mabadiliko, Kimbia.
NB; Kumbuka Kuwa Kuna Mtu Maalum
Kapangwa Kwa Ajili Yako, Muda Utafika Tu Na Utapata Furaha Unayoitafuta,
Usiogope Kuanza Upya Kama Ulipo Hapakufai.
Leave a Comment