HAKUNA MAFUNZO KWA MADEREVA KILA BAADA MIAKA MITATU

Mpinga
Kamanda wa Pol litakapokamilika kwa mchakato wake. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa madereva nchini, Clement Masanja.  isi wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, DCP  Mohammed R. Mpinga – DCP (kulia) akitoa maelezo ya kiutalaamu juu ya suala la kusoma kwa madereva ambalo kwa sasa suala hilo limesitishwa hadi hapo. Taarifa hiyo aliitoa jijini katika ukumbi wa habari MAELEZO, jijini Dar es Salaam.
TAARIFA KWA UMMA
 Hivi karibuni nchi yetu imekumbwa na Migomo ya Madereva iliyopelekea adha kubwa kwa wananchi pamoja na kuathiri uchumi wa nchi yetu. Mojawapo ya madai ya madereva ilihusiana na kukataa kwenda kusoma pamoja na gharama ya mafunzo kudaiwa kuwa Ths 560,000/=.
Ndugu Waandishi wa habari,
Katika kukabiliana na ajali za Barabarani, Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani kiliona kuna upungufu katika eneo la Ukaguzi wa magari, muenekeno wa magari makubwa yanapo haribika usiku, ulipaji wa faini ya papo kwa papo, na elimu duni au umuhimu wa kusoma kwa madereva kila baada ya kipindi fulani.
Hivyo moja ya kanuni iliyolalamikiwa sana na madereva na kuwa sababu mojawapo ya migomo, ni ile inayowataka madereva wa mabasi na malori kwenda kusoma, kuangaliwa afya kisha kujaribiwa kila baada ya miaka 3 na pia kuwataka madereva wa magari mengine kuangaliwa afya na kujaribiwa kila baada ya miaka 6 ( The Road Traffic ( Examination and Re-Testing of Drivers) Regulation GN No 31 ya 30/01/2015. Mchakato wa kuandaa kanuni hii ulianza tokea mwanzoni mwa mwaka 2014 na kupitia hatua mbali mbali ulioshirikisha wadau toka TRA, SUMATRA, NIT, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, TABOA, TATOA, Vyama vyama vya Madereva n.k.
Ndugu Waadishi wa Habari,
Kimsingi hitaji la kupata mafunzo ya muda mfupi (refresher course) kila baada ya miaka 3 lililoko kwenye kanuni hizi linawahusu madereva wenye leseni za madaraja E, C, C1, C2, na C3 ambapo wanaweza kupata mafunzo hayo muda wowote kabla leseni haijafikia muda wake wa kuhuishwa. Halikadhalika kanuni hizi zimeweka hitaji la dereva yeyote anayetaka kupata leseni daraja E kupata mafunzo ya kuenda magari makubwa na zinampatia mamlaka Mkuu wa jeshi la Polisi (IGP) kumwamuru dereva yeyote kurudi shule endapo ataonekena kufanya kitendo  hatarishi. Aidha katika kanuni hizi, hakuna chuo kilichotajwa kutoa mafunzo ya “Refresher” yatakayochukua siku 3 hadi 5 na wala matayarisho ya mtaala wake hayajakamilika.
Ndugu Waandishi wa Habari,
Nichukue nafasi hii kuwajulisha madereva wote wa vyombo vya moto na wananchi kwa ujumla, Mwaka huu hakutakuwa na mafunzo au kutakiwa kwenda kusoma kwa mujibu wa mahitaji ya kanuni hizi. Mitaala ya mafunzo haya mafupi haijakamilika na shule zitakazo husika hazijaanishwa aidha ada za mafunzo hazijapangwa na ada ya Ths ya 560,000/= haijawahi kutamkwa na serikali.
Kwa madereva ambao leseni zao zimekwisha  au zitaisha katika kipindi hiki watabadilishiwa/kuhuisha leseni zao kwa utaratibu wa zamani bila kuulizwa vyeti vya mafunzo mafupi (Refresher course).
Mwisho niwatake madereva wote wawe na uvumilivu kwa matatizo na changamoto zao kwani kamati ya Kudumu ya kutatua matatizo katika sekta ya usafirishaji iliyoundwa na Mhe. Waziri Mkuu itayapatia ufumbuzi wa kudumu.
Imetolewa:-
 Mohammed R. Mpinga – DCP
KAMANDA WA POLISI
KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI ( T )
 13th  May, 2015

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.