Dk Utaro mwenyekiti mpya JET

DSC06254
Mwenyekiti mteule wa Chama cha Waandishi wa Habari Mazingira Tanzania (JET), Dk.Elen Utaro akitoa shukrani zake kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchanguzi wa chama hicho kwa kumpatia kura za kutosha na amewataka wampe ushirikiano wa kutosha ili kukiendeleza mbele chama hicho.
DSC06248
Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wa Mazingira Tanzania (JET), Aisha Dachi, akizungumza kwenye mkutano mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mazingira ambapo alitangza hagombei tena nafasi hiyo kwa madai anachukia ‘Ukurunzinza’. Kulia ni Katibu Chrysostom Rwemamu na kushoto ni Katibu mtendaji JET John Chikomo.
DSC06238
Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa uchanguzi wa Chama cha Waandishi wa Habari wa Mazingira Tanzania (JET) waliohudhuria mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Lion Sinza jijini Dar-es-salaam.
DSC06237
Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET) aliyemaliza muda wake, Aisha Dachi, akimkabidhi Frank Kimaro (54) mkazi wa mkoa wa Kilimanjaro, tuzo na shilingi milioni moja kwa juhudi zake za kutunza vyanzo vya maji.

Na Nathaniel Limu, Dar es Salaam
MKUTANO mkuu wa uchanguzi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET), umemchangua Dk.Elen Utaro, kuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Dk.Utaro ambaye alikuwa  mgombe pekee katika nafasi hiyo, alipata kura za ndio 32 dhidi ya kura 13 zilizomkataa,wakati makamu mwenyekiti Ali Haji Hamad wa Zanzibar alipata kura 41 za ndio na tatu zilimkataa.
Mkutano huyo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Lion jijini Dar-es-salaam na kusimamiwa vema na Mwanasheria Emmanuel Masawe, uliwachangua wajumbe wa bodi na kura zao kwenye mabano kuwa ni Lea Moshi (43), Andrew Chale (39), Judica Lasai (35), Bakari Kimwaga (34),na Singi Mugumia (28). Jumla ya wajumbe 44 walipiga kura.
Awali Makamu Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Aisha Dachi ambaye alisimamia mkutano huo mkuu wa uchanguzi, alisema yeye binafsi hakutaka kutetea nafasi yake hiyo,kwa madai kwamba hapendi mtindo wa ‘Ukurunzinza’.
Dachi alisema ‘Ukurunzinza’ pamoja na madhara yake mengi, pia unabinya demokrasia kwa vile unawanyima watu/wanachama wengine kupata nafasi ya kuonyesha uwezo wa kutumikia chama chake.
“Ninyi wenzetu tuliokuwa pamoja katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita,endelelezeni majadiliano mengi ambayo tumeyaanzisha na tulikuwa hatujayapatia majawabu.Endelelezeni na simamieni kwa pamoja na wenzenu wapya suala la kupata nyumba ua makazi ya chama chetu cha JET na zaidi hakikisheni mnaongeza wanacha wengi zaidi kadri mtakavyoweza”,alisema Dachi ambaye anaitumikia TBC taifa.
Awali Katibu wa JET, Chrysostom Rweyemamu, alitaja baadhi ya shughuli kubwa zinazotarajiwa kutekelezwa kwa kipindi cha mwaka wa 2015 kilichobakia,kuwa ni kusimamia utekelezaji wa miradi iliyopo na mabayo haijaiva ya Ardhi Yetu Ajenda Yetu,mradi wa Mama Misitu na mafuta ya gesi.
Alitaja shughuli nyingine kuwa ni kuandaa ziara tano za waandishi wa habari kutoka wilaya za Mufindi , Kilwa, Rufiji, Kilolo na Mbarali kwa ajili ya kukusanya ushahidi na taarifa za mabadiloko hasi na chanya ya utekelezaji wa mradi wa Ardhi Yetu Ajenda Yetu
TUKUTANE FACEBOOK KWA KUBOFYA HAPA>>>FB<<<

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.