Mtambo wa kuzalisha Bunduki za kienyeji wakamatwa


Mtambo wa kutengeneza silaha wakamatwa  Rukwa.
Mtambo wa kutengeneza silaha wakamatwa Rukwa.

Watuhumiwa 19  wamekamatwa mkoani Rukwa   na  mtambo wa mtambo wa kutengeneza bunduki za kienyeji pamoja na silaha za aina mbalimbali zikiwemo bunduki 30 na risasi 231.
Silaha hizo  zimekamatwa  kufutia msako uliofanywa na Polisi ambapo mbali na silaha hizo waliweza pia kukamata meno   na  mikia miwili ya tembo.
Akizungumzia tukio hilo  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema jana mjini kuwa silaha hizo zilikamatwa kutokana na operesheni ya kupambana na visa vya ujangili na uhalifu mwingine katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa huo.
Ameongeza  kuwa silaha hizo zilizokamatwa zinasadikiwa kutumika katika matukio ya  kijangili na uhalifu mwingine ambapo baadhi ya bunduki zimegundulika kuwa zinamilikiwa kihalali.
Kwa upande wa silaha  zilizokamatwa ametaja kuwa  ni  bunduki aina ya shotgun 8, rifle 8, magobori 4, bunduki 6 aina ya shotgun zilizotengenezwa kienyeji, risasi 5 za SMG, risasi 53 za rifle na risasi 173 za shotgun.
Watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote baada ya uchunguzi wa awali wa kukamilika.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.