ULIWAHI KUJIULIZA KUWA NJIA UNAYOTAMANI AU ULIYOCHAGUA NI SAHIHI KWAKO, UNAZIJUA ISHARA ZAKE? SOMA UJIELIMISHE.

"Je, niko katika njia sahihi?"
Kama,
 umewahi kujiuliza hili swali,
uko karibu 
kuipata njia yako sahihi.
Wengi,
 tunajihusisha katika shughuli mbali mbali bila kujua 
kama njia tunayoifuata/tuliyochukua
 ni sahihi au 
si sahihi kwetu.
Ulishawahi kuamka usiku mnene,
huku ukijiuliza kama njia uliyaochagua ni sahihi kwako au la?

Wengi tunajiuliza,
kuwa njia sahihi maana yake ni nini?

Kujiuliza swali hili,
 ni hatua kubwa sana 
kupiga katika maisha yako ya 
kutafuta shughuli sahihi ya kufanya.
Fahamu wazi,
 kuwa unaanza kujitambua,
na ni ishara mojawapo ya kujua 
mahitaji gani ni muhimu kwako.

Yawezekana,
ukawa unalipwa vizuri,
una mazingira mazuri ya kazi,
au una 
vifaa vyote vya kufanyia kazi zako.
Linapokuja
 suala la upo sehemu sahihi au 
sio sahihi 
masuala hayo niliyotaja hapo juu
 huwekwa kando.

Ishara za kuangalia kama upo njia sahihi katika shughuli unayofanya:

1.MUDA HAUKUTOSHI

Unapokuwa unafanya hiyo shughuli,
unaona muda kama unapaa.
Kwa kuwa
kwako si kazi tu bali unafurahia 
kila dakika ya 
kitu unachofanya.
Na unapokuwa mbali 
na shughuli yako au 
hata ukiwa umelala unatamani asubuhi ifike ili urudi tena eneo lako la kazi.

2.UNAPOTEZA MUUNGANIKO NA MATUKIO YA NJE YA KAZI

Unapokuwa mzigoni unahisi kama unasafiri dunia ya kipekee,
na unapoteza mawasiliano na dunia inayokuzunguka.
Unaweza  ukawa unaongeleshwa na watu na usiwasikie kabisa,
 kwa kuwa akili yako yote imetekwa 
kwa muda huo na muda mwengine hata kula unasahau.

3.UNA IMANI NAYO MOYONI

Moyoni una imani kuwa
 hii ndiyo kazi uliyoumbwa kuifanya na hakuna 
atakayeweza kukubadilisha mawazo 
na imani yako
 uliyonayo juu ya shughuli hiyo.

4.UNA MAONO NA SHUGHULI HIYO

Una maono ya wazi kabisa ,
ya nini 
unataka kupata baada ya muda fulani, 
na hata kama kuna 
vikwazo vinajitokeza bado 
unanguvu za kutaka kufikia 
lengo lako.

5.HAUKATI TAMAA

Hata kama kuna watu, 
au mazingira 
yanataka kukurudisha nyuma
 bado hutaki kukata tamaa na 
shughuli yako.

6.UNAFURAHIA CHANGAMOTO

Pamoja na changamoto zinazojitokeza
 mara kwa mara 
unafurahia uwepo wake kwani zinakupa 
uzoefu mpya ambao mwanzo
 hukuwa nao.

7.WATU WANAKUUNGA MKONO

Watu kadhaa watachukua muda wao,
 kuwasiliana na wewe 
ili kukupa msaada na muongozo wa 
shughuli yako.
Hata wewe mwenyewe huelewi watu hawa wanakujaje katika maisha yako
 lakini
 wanakuja na msaada mkubwa sana kwako.

8.UNACHOFANYA KINALETA MABADILIKO YA KWELI KATIKA MAISHA YA WENGINE

Wewe unaweza ukaona 
unachofanya ni kitu kidogo lakini kuna 
watu kinawasaidia sana,
na mrejesho wao 
utakupa picha halisi ya jinsi unavyogusa maisha ya watu wengine.

NI VYEMA UKAANZA KUJITAFAKARI SASA,
KAMA NJIA UNAYOTAMANI 
AU ULIYOCHUKUA 
NI SAHIHI AU LA.

 HII ITAKUSAIDIA KUKUEPUSHA NA UPEPO USIO SAHIHI.

NA KUANZIA LEO,
 TAMBUA KUWA NJIA SAHIHI
 NDIO ITAKAYOKUPA MAFANIKIO YA KWELI KATIKA MAISHA YAKO.
BOFYA HAPA UJIONEE MAAJABU YA FACEBOOK

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.