WAZIRI MKUU KUANZA ZIARA MKOANI RUVUMA

maj2
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa   anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya siku nne mkoani Ruvuma, ambapo atawasili mkoani  hapo  leo saa tisa alasiri.
Baada ya Waziri Mkuu kuwasili Uwanja wa Ndege wa Songea, atapokelewa na viongozi wa Chama na Serikali, pia atakwenda Ikulu kupokea taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Ruvuma.
Aidha, siku ya jumatatu  atakuwa na shughuli za kufungua  tawi la Benki ya Posta mjini Songea, kukagua  maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula  (NFRA) kanda ya Songea na kukagua  makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.
Siku inafuata atatembelea na kukagua Hospitali ya Rufaa ya mkoa, na baadaye kuzungumza na watumishi wa hospitali  hiyo.
Siku ya nne ya ziara yaani jumatano, Waziri Mkuu atafanya majumuisho ya ziara mkoani humo, kabla ya kuagana na viongozi wa Chama na Serikali na kurejea Dar es Salaam.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.