ISHARA 10 ZA MWANAUME ALIYEZAMA KATIKA PENZI LAKO.
Kabla ya yote CLICK HAPA
Mwanaume anayezama katika penzi huanza kuonesha sifa na
tabia maalumu.
Kwa kawaida, wanaume na wanawake huonesha na kuelezea
hisia zao kwa namna inayotofautiana kabisa, hivyo, wakati mwingine ni vigumu
hasa kujua hisia za mumeo. Kila mwanaume ana njia yake ya kuonesha mahabba
yake, lakini hizi ni ishara ndogo za jumla ambazo hutoa mwelekeo unaoonesha
wakati ambao wanaume wanakuwa wamezama kwenye penzi.
1. HUWA MAKINI
Mwanaume anayependa humakinika unapokuwa
karibu naye. Je, anakutazama machoni na kuzungumza nawe moja kwa moja hata kama
kuna watu karibu yenu? Hata kama ukiwa mbele ya watu haachi kuelekeza umakini
wake kwako.
2. HUKUFANYA KUWA
KIPAUMBELE
Hakuna kitu muhimu sana kwa mwanaume
analiyependa kama kuwa na mwanamke anayemfanya awe na shauku. Bila shaka atakuwa
na kazi zake, atakuwa na marafiki, atakuwa na mambo kayaya anayoyapenda, lakini
umuhimu anauweka kwako, anaweka umuhimu wa kuwa pamoja nawe. Anapokuona, hujawa
na furaha.
3. JUHUDI NA HARAKATI
ZA KUKUVUTA
Mwanaume anayetaka kuuvuta moyo wa mwanamke
hufanya juhudi za kumvutia. Anataka mwanamke anamuone kuwa yeye ni mtu maalumu,
amuone kuwa ana upekee na umaalumu unaoweza kumvutia na kumvuta kwake.
4. HUKUCHEKESHA
Anapokuwa amekupenda, anataka umakinike. Miongoni
mwa njia bora kabisa za kufanya hivyo ni kukuchokoza. Hukupa majina ya utani,
hukufanyia utani…. Anafanya chochote ili kukufanya utabasamu. Ni njia yake ya
kukuonesha kuwa ni mcheshi kwako.
5. HUKUSIFU
Mwanaume aliyezama kwenye upendo anaweza kuwa
mchunguzaji sana; hii ni sehemu ya namna anavyotaka kuuvuta moyo wako. Hilo linaweza
kuonekana kwa namna anavyokumwagia sifa. Huchambua muonekano wako na kuutambua
urembo wako maridhawa.
6. HUTAFUTA NJIA YA
KUTOA
Mwanaume anapokuwa kwenye kilele cha mapenzi,
hutafuta vitu vidogo vidogo anavyoweza kukupatia ili kuonesha mapenzi kwako
kama vile zawadi ndogo ndogo na kadhalika.
7. HUONA WIVU
Sio wanaume wote wenye wivu, na wivu
uliopindukia sio mzuri, lakini mwanaume wako hapendi uugawe umakini wako kwa
wanaume wengine, hapendi uwatazame wanaume wengine. Hilo linapotokea, huanza
kukosa amani na kuhisi kitisho dhidi ya himaya ya moyo wake.
8. HUJIZUNGUMZIA
Wanaume hupata wakati mgumu kuzungumzia hisia
zao. Kama anafunguka na kujizungumzia mbele yako, inaonesha kuwa anakuamini. Hii
ni ishara kuwa uhusiano wako ni muhimu sana na hafanyi mzaha.
9. ANATAKA MARAFIKI
ZAKE WAKUONE
Anaona fakhari kuwa na wewe. Kwa ajili hiyo,
anataka dunia ikuone, ikiwa ni pamoja na marafiki zake na familia yake.
10. ANAKUJUMUISHA
KWENYE MIPANGO YAKE YA BAADAYE
Bila shaka miongoni mwa ishara kubwa kabisa
zinazoonesha kuwa mwanaume amezama kwenye mapenzi ni pale anapokujumuisha
kwenye mipango yake ya baadaye. Hiyo inaonesha kuwa anataka kuwa nawe daima.
Leave a Comment