JIEPUSHE NA MARAFIKI WA AINA HII KAMA UNATAKA KUFANIKIWA KIMAISHA

 
 
Mafanikio ya mtu yapo mikononi mwake, pia ni jinsi anavyojitazama kwa mtazamo wa wengine na kujichukulia bila kuangalia wengine wanasemaje kuhusu maamuzi yake.
Mwanadamu ana nguvu ya asili ya kufanya machaguo.Nikimnukuu Hayati Baba wa Taifa la Tanzania- Mwalimu Julius K.Nyerere aliwahi kusema-Maisha ni kuchagua.Inategemea unaamua kuchagua nini kwa vile unavyotaka uwe. Jinsi ulivyo sasa kimaisha ni kutokana na maamuzi/machaguo yaliyofanyika siku zilizopita. 

Tunaweza pia kuchagua marafiki ili tushirikiane katika kupambana na changamoto za maisha.Marafiki hao wanaweza kuchangia au kudidimiza mafanikio yako kama umakini hautachukua nafasi yake.Inategemea ni aina gani ya rafiki unachangamana naye.Leo naomba nikujuze aina ya marafiki unaopaswa kujiepusha nao.Utawatambua kwa maneno yao na mazoea yao/tabia zao.

1.MARAFIKI WASIOTAKA KUELEZA YAO…ILA WANA UCHU WA KUJUA YAKO
Aina hii ya marafiki ni hatari sana…mara nyingi hukudodosa kujua mipango yako, mwisho kukukatisha tamaa, wakati huo huo wanatumia mawazo yako waliyoyabeza!

2.RAFIKI ANAYEJIJALI YEYE TU…HAJALI MUDA, MCHANGO WAKO
Hii ni hali ya ubinafsi inayoweza kuufanya urafiki uwe wa upande mmoja.Pia kupelekea mmoja kujiona ni zaidi kuliko mwingine.(Itambulike kuwa urafiki ni kufaidiana na kusaidiana…kila mmoja ana mtegemea mwenzake).

3. MARAFIKI WAENDEKEZA STAREHE KULIKO KAZI
Waepuke marafiki wavivu wasiopenda kufanya kazi na mwisho wa siku wanataka mtoke mkatumie ulizozichuma.Kundi hili litakurudisha nyuma kimaendeleo.Na kundi hili linalokuwa la kwanza kukukimbia ukiishiwa.Hakuna urafiki wa kweli kwenye kundi hili!

4. RAFIKI ANAYESEMA YAKO YA SIRINI KWA WENGINE
Muogope rafiki ikiwa umembaini! Huyu aweza kuwa mchonganishi.Unajua kuwa watu wengine wakielezwa siri huwa inawawasha miyoni mwao…hivyo huileza kwa wengine kirahisi sana.Mtambue rafiki wa aina hii…epuka kumueleza siri zako!

5.RAFIKI ANAYEPENDA KUKUKOPA HALAFU HAKULIPI…UKIMDAI UGOMVI MKUBWA!
Kundi hili hupenda kutumia njia ya urafiki kujineemesha kirahisi wakati huo huo likileta ugomvi ndani ya urafiki.Ukiiona umemkopesha rafiki yako pesa halafu amekaa kimya hadi siku aliyoahidi kukulipa ujue…………..ukitaka msigombane usidai! Ila ujue kuwa anakurudisha nyuma kimaendeleo, si unajua tena pesa haitoshi!

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.