TAARIFA YA HABARI YA PLANET FM HII HAPA

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imefanikiwa kukusanya sh. bilioni 83.4 kufikia mwaka 2013/2014 ambazo zinatokana na shughuli mbalimbali zilizofanywa na Idara ya Uhamiaji.
..............................
Serikali ya Tanzania, kwakushirikiana na mashirika  manne ya kimataifa leo wamezindua mpango wa pamoja wa kukomesha ukatili dhidi ya watoto nchini.
......................................
Serikali imefanikiwa kutoa kiasi cha shilingi bilioni moja na milioni 750, kama fidia kwa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha mara baada ya kuchukua mradi wa Halmashauri hiyo, ujulikao kama Laki Laki kwa ajili ya kujenga miji ya kisasa katika maeneo hayo.
                           KIMATAIFA
Mataifa ya nchi za Afrika Mashariki yameidhinisha kupelekwa kwa kikosi cha wanajeshi 5,500 nchini Sudan Kusini ili kumaliza mgogoro wa kisiasa ambao umekuwa ukiendelea kwa wiki kadhaa nchini humo.
..............................
Watu watatu wameripotiwa kuuawa katika wimbi jipya la maandamano ya kuipinga serikali ya Ukraine, tukio ambalo limechochewa na mgogoro wa kisiasa wa nchi hiyo, uliodumu kwa miezi miwili sasa.
.........................
Shirika la kimataifa la kuhudumia Watoto la UNICEF, limeanza kuandaa kampeni ya chanjo kwa Watoto zaidi ya milioni 1na laki 6 ili kupambana na ugonjwa wa Surua uliojitokeza nchini Guinea.
                              
                                                .... MWISHO....






No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.