Watu watatu wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoani morogoro, kwa kosa la kula njama na kumfanyia ukatili mtoto Nasra Rashidi mwenye umri wa miaka 4 mkazi wa Kiwanja cha ndege Manispaa ya Morogoro. 

Akisoma mashitaka hayo, msoma mashitaka wa mahakama hiyo Bi. Anganile Msyani amesema watuhumiwa wametenda makosa kati ya mwezi Desemba mwaka 2010 na May 2014, ambapo walimuweka mtoto huyo ndani ya boksi kwa muda wa miaka minne kitendo kilichosababisha utapiamlo, kuvunjika kwa miguu na mikono pamoja na udhaifu wa mwili kwa mtoto huyo.

Aidha, watuhumiwa hao ni Mariam Saidi mwenye umri wa miaka 38 kabila Myao, Mtonga Omary miaka 30 Mluguru wote wakazi wa Kiwanja cha ndege na Rashidi Mvungi miaka 47 Afisa Elimu Morogoro vijijini mkazi wa Lukobe wametenda makosa hayo yaliyopo kwenye kesi namba 79 ya mwaka 2014.


Pia imeelezwa kuwa, upelelezi umekamilika na dhamana iko wazi kwa kila mshitakiwa, kuwa na wadhamini wawili wa kuaminiwa pamoja na shilingi milioni tano za kitanzania kwa kila mmoja, ambapo kesi hiyo itatajwa tena mnamo tarehe 9 mwezi wa 6 mwaka huu.

                                     

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.