BREAKING NEW: 

WAMBURA BASI TENA SIMBA, KAMATI YA TFF YAMTUPA



Taarifa zinaeleza Michael Richard Wambura amepigwa chini na kamati ya rufaa ya TFF.

Kamati hiyo imeungana na kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya Dokta Damas Daniel Ndumbaro ‘DDN’ ambayo ilimpiga chini Wambura kugombea Simba baada ya kubaini alipiga kampeni kabla ya muda.

Rufaa yake aliyokata katika kamati ya rufaa ya TFF ilisikilizwa leo kwenye hoteli ya Courtyard jijini Dar.

Taarifa zinaeleza wajumbe wa kamati walikuwa wanne baada ya Jaji Jilius Lugziya kuomba udhuru, hivyo wanne wameamua kuwa kweli Wambura alikuwa anakosa.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.