MKUU WA KITUO CHA POLISI (OCS) AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUKUTWA AKIMBAKA MWANAFUNZI...!!!!

ALIYEKUWA Mkuu wa Kituo cha Polisi Nyamboge katika wilaya na Mkoa wa Geita E:2837 D/C Venance anashikiliwa na Polisi mkoani humo kwa tuhuma za kukutwa akimbaka mwanafunzi.
 
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka katika eneo la tukio, Mkuu huyo wa Kituo alimfanyia unyama huo mwanafunzi huyo (18), anayesoma kidato cha Nne katika shule ya sekondari Nyamboge.

Imeelezwa kuwa juzi mkuu huyo wa kituo alimtuma mmoja wa ‘vijana’ kwa ajili ya kuzungumza na mwanafunzi huyo, ili akubali kufanya mapenzi naye mapenzi lakini mwaanafunzi huyo alikataa kwamba hawezi kwenda nyumbani kwake (Askari).
 
“Mwanafunzi huyo alimweleza kijana aliyetumwa kwamba hawezi kwenda nymbani kwa OCS,na kwamba kama anamhitaji amfuate chumbani kwake (Geto) ili akapate hicho anachokihitaji….” shuhuda aliieleza 
 
“Baada ya OCS kupata majibu hayo alikwenda hadi chumbani kwa mwanafunzi huyo ambaye amepanga chumba kutokana na kuishi kijiji kingine mbali na ilipo shule hiyo, lakini kumbe alikuwa amekwishawaeleza wenzake juu ya namna anavyotendewa na OCS….” shuhuda wetu alizidi kufafanua.
 
Inadaiwa kuwa OCS alifika chumbani hapo majira ya saa mbili usiku na baada ya kuingia ndani mmoja wa vijana anayesoma na mwanafunzi huyo ambaye alikuwa ameombwa na mwanafunzi wa kike kumsaidia alikwenda kufunga mlango kisha kupiga yowe kuomba msaada.
“OCS aliposikia yowe aliamua kuvunja mlango lakini wakati anatoka nje akakamatwa na wananchi ambao tayari walikuwa wameitikia yowe na kuanza kumshambulia; hata hivyo polisi waliwahi kufika eneo la tukio na kumuokoa…..” chanzo chetu kilieleza.
 
Kamanda wa Polisi Mkoani Geita, Joseph Konyo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tayari jeshi hilo limefungua jalada la uchunguzi dhidi ya mtuhumiwa ingawa hatua ya kwanza waliyochukua ni kumvua cheo alichokuwa nacho.
 
“Ni kweli hilo tukio lipo, tunaendelea kumshikilia hadi pale tutakapojiridhisha na kila aina ya ushahidi tunaouhitaji; tayari tumechukua hatua za awali ikiwa ni kumvua nyadhifa yake aliyokuwa nayo na tumeshaanzisha mashitaka ya kijeshi dhidi yake…” Kamanda Konyo alisema
 
“Taarifa tulizopokea ambazo hata yeye amekiri ni kwamba kweli alikuwa akihitaji mahusiano na mwanafunzi huyo na mbinu aliyoitumia ni baada ya kuamuru mwanafunzi huyo aachiwe kutokana na mashitaka yaliyokuwa yakimkabili kituoni hapo….” Konyo aliongeza.
 
Akifafanua, Kamanda Konyo alisema askari wawili wa kituo hicho walimtia mbaroni mwanafunzi huyo kwa tuhuma za kufanya mapenzi na mwalimu wake na kwamba walipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba mwanafunzi huyo alikuwa anatembea na mwalimu wake.
 
Alisema baada ya suala hilo kufikishwa mbele ya OCS alimuita mwanafunzi na kumwambia anamsaidia ili afutiwe shitaka lakini akaweka sharti la kufanya mapenzi na mwanafunzi huyo.
 
“Inavyoonekana mwanafunzi alikubali kwa sababu alikuwa kwenye matatizo lakini alipotoka akaanza kumpiga chenga OCS na ndipo akaamua kufanya uamuzi huo kwa sababu hakupendezeshwa; kuna madai kwamba alipoingia alianza juhudi za kumbaka lakini wananchi waliwahi kufika madai ambayo tumeanza kuyachunguza…” Aliongeza kamanda Konyo.
 
Kwa mujibu wa kamanda Konyo Askari huyo atashitakiwa kijeshi na baada ya kesi yake kukamilika atafikishwa katika mahakama za kiraia.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.