KOCHA NOOIJ KUTAJA KIKOSI STARS
Kocha
Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij kesho (Novemba 5 mwaka huu) atatangaza
kikosi cha timu hiyo kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) itakayochezwa ugenini Novemba 16
mwaka huu.
Nooij
atatangaza kikosi hicho mbele ya waandishi wa habari katika mkutano
utakaofanyika saa 4.30 asubuhi kwenye ofisi za TFF zilizoko ghorofa ya
tatu, Jengo la PPF Tower jijini Dar es Salaam.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na
Swaziland, mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Somhlolo jijini
Mbabane.
Leave a Comment