10 wafariki kwa ajali ya basi la Unique Shinyanga


Ajali iliyohusisha basi la Unique mkoani Shinyanga.
Ajali iliyohusisha basi la Unique mkoani Shinyanga.
Basi la kampuni ya Unique mara baada ya kupata ajali.
Basi la kampuni ya Unique mara baada ya kupata ajali.
Askari wakitoa msaada katika eneo la ajali iliyohusisha basi l akampuni y aUnique.
Askari wakitoa msaada katika eneo la ajali iliyohusisha basi l akampuni y aUnique.
Baadhi ya majeruhi wakiolewa katika eneo la ajali.
Baadhi ya majeruhi wakiolewa katika eneo la ajali.

Basi la kampuni ya  Unique lenye namba za usajili T148 BKK likitokea jijini Mwanza kwenda Tabora limegongana uso kwa uso jana alasiri  na lori la kampuni ya Cocacola katika kijiji cha Ibingo kata ya Samuye mkoani  Shinyanga.
Katika ajali hiyo watu 10 wamefariki na  50 wamejeruhiwa. Majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga.
Kwa mujibu wa baadhi ya abiria walionusurika katika ajali hiyo wamesema kuwa dereva wa lori alikuwa anaendesha gari katikati ya barabara huku dereva wa basi akiwa katika mwendo kasi na katika kukwepa, basi hilo aligonga tela la lori kisha kupinduka.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha  amethibitisha kutokea tukio hilo lilihusisha    watu 10 kupoteza maisha katika ajali hiyo kati yao 9 walifariki dunia papo hapo huku majeruhi 50 wakiwemo wanawake 13, wanaume 36 na mtoto mmoja wa kiume wakiwa wanaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

No comments

Theme images by sbayram. Powered by Blogger.