Utingo ajaribu kuendesha gari....kilichomkuta ni balaa
Utingo aliyejaribu kuendesha daladala amekatisha maisha ya
mwanafunzi mmoja na kujeruhi mtu mwingine mmoja, huku wengine wakiponea
katika tundu la sindano.
Katika ajali hiyo ya kusikitisha, ndugu wa mwanafunzi huyo
aliyefariki wamesimulia kuwa ndugu yao na watu wengine walikuwa
wamesimama katika kituo cha mabasi cha Makumbusho ndipo basi hilo
lilipokuja na kusimama.
Kwa mujibu wa shuhuda amedai kuwa baada ya dereva kuegesha basi
lake na kushuka utingo huyo alijaribu kusogeza gari lakini likamshinda
na kujikuta likiwaparamia watu waliokuwa wamesimama kituoni hapo na
kupeleka maafa, simanzi, maumivu na mshtuko kwa watu wasiokuwa na hatia.
Imesekana kuwa baada ya ajali hiyo utingo huyo ambaye jina lake
halikuweza kujulikana mara moja alifanikiwa kutoroka huku gari hilo
lililopelekea ajali hiyo kupelekwa kituo cha polisi cha oysterbay ambako
jalada limefunguliwa.
Marehemu wa ajali hiyo ametambuliwa kama Naomi Lawrence Mwalusako,
mtoto wa mchezaji maarufu wa zamani wa klabu ya Yanga na Taifa stars
ambaye pia ameiongoza Yanga kama Katibu Mkuu.
Cha kusikitisha zaidi ni kuwa marehemu Naomi, ndio alikuwa
amemaliza tu mitihani yake ya kidato cha sita huku yeye na familia yake
walikuwa na mategemeo na ndoto kubwa kwake.
Zaidi ya marehemu Naomi, mtu mmoja alijeruhiwa sana katika ajali
hiyo na hadi sasa amelazwa katika hospitali ya Mwananyamala huku mwili
wa Naomi nao ukiwa umhifadhiwa katika hospitali hiyo pia.
Leave a Comment